Katibu wa halmashauri kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi, Nape M. Nnauye akiongea katika moja ya mkutano na waandishi wa habari |
Katibu wa halmashauri kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi, Nape M. Nnauye |
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi ya Ubunge, Uwakilishi na Udiwani ndani ya CCM ulioanza tarehe 15/07/2015 unaendelea vizuri na unakaribia katika hatua za mwisho za uteuzi. Kwa nafasi ya Ubunge na Uwakilishi tunategemea kufanya uteuzi tarehe 13/08/2015.
Kutokana na mchakato huo, kuna baadhi ya maeneo kuna malalamiko ya hapa na pale. Iwapo kuna mwanachama ambae hakuridhaka na mchakato ulivyoendeshwa kwenye eneo lake apeleke malalamiko yake kwenye ngazi ya juu ya ngazi iliyosimamia mchakato husika.
Pamekuwa na utamaduni unaojengwa wa makada wetu kulalamika barabarani na wakati mwingine kushawishi wanachama kulalamika kwenye vyombo vya habari na kwingineko, utaratibu huo sio wa chama chetu, Chama kinazo taratibu za kushughulikia malalamiko yatokanayo na michakato hii. Tunashauri taratibu hizo zifuatwe. Katika kufikia hatua hiyo wanachama wanaombwa kuwa watulivu.
Kumetokea pia wimbi la matapeli wanaotumia majina ya viongozi, na baadhi yao wamesajili simu zao kwa majina ya viongozi wakizitumia kwa kuwatapeli wagombea wanaotafuta nafasi za uongozi kwa kuwaahidi watatumia nafasi zao kuwapitisha majina yao katika vikao vinavyotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Chama Cha Mapinduzi kinawatahadharisha wanachama ambao watapata simu hizo kuzipuuza na kuwa waangalifu dhidi ya matapeli hao.
Hakuna njia ya mkato kupata uteuzi ndani ya CCM zaidi ya kufuata kanuni na taratibu za Chama. Njia yoyote ya mkato ni utapeli na hauna nafasi ndani ya CCM.
Zipo taarifa za uhakika kuwa kuna baadhi ya makundi ndani ya UKAWA yamepanga na wameanza kuratibu zoezi la kutengeneza kadi feki (za bandia) za CCM na kuzigawa kwa watu wao ili baadaye asipopita mgombea wao ionekane Wana CCM wanakihama chama chao kwa kuzirudisha kadi hizo kwenye shughuli mbalimbali za vyama hivyo vinavyounda UKAWA.
Hakuna njia ya mkato kupata uteuzi ndani ya CCM zaidi ya kufuata kanuni na taratibu za Chama. Njia yoyote ya mkato ni utapeli na hauna nafasi ndani ya CCM.
Zipo taarifa za uhakika kuwa kuna baadhi ya makundi ndani ya UKAWA yamepanga na wameanza kuratibu zoezi la kutengeneza kadi feki (za bandia) za CCM na kuzigawa kwa watu wao ili baadaye asipopita mgombea wao ionekane Wana CCM wanakihama chama chao kwa kuzirudisha kadi hizo kwenye shughuli mbalimbali za vyama hivyo vinavyounda UKAWA.
Taarifa hii inafanyiwa kazi ndani ya chama na kwa wakati huu tunawaomba wananchi wawe makini na waangalifu wasije ingizwa kwenye uhalifu huu usiokuwa na tija.
Kwa taarifa hii, tunawaomba wanachama wa CCM na wapenzi wa Chama chetu kutokuwa na hofu na hila hizo na wawe macho kuzibaini mbinu hizo chafu na kuzitolea taarifa kwa vyombo vinavyohusika.
Kwa taarifa hii, tunawaomba wanachama wa CCM na wapenzi wa Chama chetu kutokuwa na hofu na hila hizo na wawe macho kuzibaini mbinu hizo chafu na kuzitolea taarifa kwa vyombo vinavyohusika.
Imetolewa na:-
Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
08/08/2015
0 comments: