CCM Kurudia Kura za Maoni katika Majimbo Matano

code         No comments

KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi(CC) imeagiza kurudiwa kwa uchaguzi   katika majimbo matano  kutokana na dosari mbalimbali zilizojitokeza katika mchakato wa kura ya maoni.




Majimbo hayo ni Makete,Busega,Ukonga,Rufiji na Kilolo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye amesema mchakato  huo utarudiwa siku ya alhamisi Agosti 13.

Amesema baada ya uchaguzi huo matokeo yatapelekwa katika vikao vinavyoendelea kwa ajili ya uamuzi.

Akizungumzia kuhusu vikao vinavyoendelea Ndugu Nape amesema vikao hivyo vinaendelea vizuri ambapo jana kikao cha kamati ya maadili kiliendelea mpaka usiku.
Amesema leo wanatarajia kumaliza  kikao cha CC ambapo kesho na kesho kutwa watamaliza na kikao 

PICHA MBALIMBALI KATIKA VIKAO VINAVYOENDELEA


Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifungua kikao cha Kamati Kuu ya CCM, leo Agosti, 11, 2015 katika ukumbi wa Jengo la White House Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Adam Kimbisa na Mzee Steven Wassira wakibadilishana mawazo ukumbini 


 Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Zakiah Meghji na Dk. Asha-Rose Migiro wakibadilishana mawazo ukumbini




Published by code

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Si vous n'avez pas eu la chance de prendre dans tous.
Follow us Google+.

0 comments:

© 2014 punguzo . Designed by Bloggertheme9
Powered by Blogger.