Slaa apeta Ukonga Kura za Maoni CCM

code         No comments


Kuelekea uchaguzi mkuu  wa Raisi, Wabunge na Madiwani utakao fanyika 25/10/ 2015  vyama  mbalimbali vya siasa vimeendelea kuchagua viongozi watakao viwakilisha vyama vyao katika ngazi ya Uraisi , wabunge na madiwani
Aliyekua Meya wa Ilala Mh. Jerry Silaa
Katika Jimbo la Ukonga jijini Dar es salaam, aliyekuwa Meya wa Ilala, Jerry Silaa amembwaga tena mrufani na mpinzani wake wa karibu Ramesh Patel kwa kupata kura 10, 965 sawa na asilimia 57.1 ya kura zote 19, 187 zilizopigwa.

Sasa Jerry silaa atakiwakilisha Chama Cha Mapinduzi CCM katika nafasi ya Ubunge  katika jimbo hilo la Ukonga.

Baada ya matokeo hayo ndugu Ramesh Patel ambaye alikubali kushindwa na kusaini fomu maalumu za chama hicho amepata kura 6, 960 sawa na asilimia 36.27.

Uchaguzi katika jimbo hilo umefanyika baada ya kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoketi mjini Dodoma hivi karibuni kuagiza urudiwe sambamba na majimbo mengine ya  Kilolo, Makete na Busega kutokana na dosari kadhaa.


Published by code

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Si vous n'avez pas eu la chance de prendre dans tous.
Follow us Google+.

0 comments:

© 2014 punguzo . Designed by Bloggertheme9
Powered by Blogger.