Mgombea Ubunge CUF Avunjiwa Nyumba Kwa Kuipa Ushindi CCM

code         No comments

Mgombea Ubunge wa wa chama cha wananchi CUF jimbo jipya la nanyamba wilaya ya mtwara vijijini, Twahiri Saidi amebomolewa nyumba yake   na wananchi  wenye hasira kali  kufuatia  kushindwa kurudisha fomu ya ubunge na kutokomea kusiko julikana huku akizima simu.

Kwa mujibu wa baadhi ya viongozi wa chama hicho na wanachi wa jimbo la Nanyamba wamesema mazingira aliyotoweka mgombea huyo  yanaonyesha wazi  kuna mchezo mchafu umefanywa ili kutoa fursa kwa  mgombea wa CCM Abdallah Chikota  kupita bila kupingwa.

Naye katibu kata wa CUF kata ya Milango Minne eneo analotoka mgombea huyo, amesema mwisho wa kuwasiliana na mgombea huyo ilikuwa majira ya saa saba akimuhimiza kuwahisha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi.

Hata hivyo anasema majibu ya mgombea huyo yalionyesha wazi kuna jambo baada ya kudai hawezi kuacha ajira yake na kuingia kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi wakati viongozi wa CUF taifa walimuaidi kumpa shilingi milioni 30 kwa ajili ya uchaguzi na wameshindwa kufanya hivyo.

Jeshi la Polisi mkoani humo limewataka wananchi kuwataja walio bomoa nyumba hiyo vinginevyo mkono wa sheria utachukua mkondo wake.


Published by code

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Si vous n'avez pas eu la chance de prendre dans tous.
Follow us Google+.

0 comments:

© 2014 punguzo . Designed by Bloggertheme9
Powered by Blogger.