Watuhumia 38 wa Ugaidi Wakamatwa , Walikua Wakitoa Mafunzo ya Kigaidi Dar, Pwani na Lindi

code         No comments

blog

Jeshi la Polisi limewakamata watu 38 wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi ambao pia wamepatiwa mafunzo ya kigaidi katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Lindi.

Sambamba na kukamatwa watu hao, polisi pia imekamata bunduki 10, risasi 300 na bomu moja la mkono.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna, Suleiman Kova ametangaza leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kova aliongeza kuwa watuhumiwa hao pia wanajihusisha na kutoa mafunzo ya kigaidi.

‘’ Hawa tumefanikiwa kuwakamata, tunawaita majambazi au magaidi kwa kuwa licha ya kufanya ujambazi pia wanajihusisha na kutoa mafunzo ya kigaidi katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Lindi,’’alisema Kamanda Kova.

Amesema kuwa polisi wamefanikiwa kuwanasa watu hao ikiwa ni operesheni endelevu ya kuwasaka wahalifu wote wanaovunja amani hapa nchini.

Silaha zilizo kamatwa
Ameeleza kuwa baadhi ya silaha zilikamatwa zikiwa zimefichwa maeneo ya Mkuranga mkoani Pwani ambapo baadhi ya silaha hizo tayari zilikuwa zimeshapata kutu.

Kamanda Kova amesisitiza kuwa polisi wanaendelea na upelelezi na ukishakamilika watuhumiwa hao watachukuliwa hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani.

Published by code

Nulla sagittis convallis arcu. Sed sed nunc. Curabitur consequat. Quisque metus enim venenatis fermentum mollis. Duis vulputate elit in elit. Si vous n'avez pas eu la chance de prendre dans tous.
Follow us Google+.

0 comments:

© 2014 punguzo . Designed by Bloggertheme9
Powered by Blogger.